Katika kile kinachoonekana ni kuendeleza wimbi la
hujuma zake za kikatili, vikosi vya utawala haramu wa Israel vimemuua
mwanamke wa Kipalestina kwa kumfyatulia risasi 50, katika mji wa
al-Khalil, katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan. Kadhalika
Wapalestina wengine wawili waliokuwa katika eneo la tukio hilo
wamejeruhiwa vibaya. Haya yanajiri siku chache baada ya jeshi katili la
Israel kumpiga risasi na kumuua kijana wa Palestina katika kituo cha
magari cha Jalama katika mji wa Jenin, katika Ukingo wa Magharibi.
Makumi ya Wapalestina wameuawa kwa risasi ya utawala huo wa Kizayuni
wakishiriki Intifadha ya 3 ya kulinda Quds Tukufu.
Aidha Wapalestina
zaidi ya 2600 wamepigwa risasi na askari wa Israel katika mwezi uliopita
pekee katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
No comments:
Post a Comment